SOMO KUHUSU VIFARANGA
Hii Imeandaliwa na:
GREYSON KAHISE
MTAALAMU WA KUKU
0769799728
0715894582
Kwa Kifupi Sana fanya yafuatayo utanishukuru
Kwanza kabisa vifaranga wanahitaji Sana Mambo yafuatayo yazingatiwe.
👉Joto
👉Chakula Safi
👉Maji Safi
👉Mzunguko mzuri wa hewa
👉Idadi sahihi ya Vyombo vya chakula na Maji
👉Randa Safi ,zisizo na vumbi, kavu
👉 Biosecurity/ usalama wa viumbe.
NISEME TU KWAMBA FUATA HAYA KWA VITENDO KABISA UTAFAULU
👉 WIKI LA KWANZA
👆Siku ya kwanza kabisa ( Glucose/Glucovet.. inategemea wametoka umbali gani wanaweza kupewa masaa 3-24).
👆 Multivitamins Mfn! Neoxychick, Chick formula ,Tetracovit Kwa siku ya kwanza Hadi ya 5 ( SIJAANDIKA DAWA HAPO).
👆Siku ya 6 huwa tunashauri wapewe maji tupu,
👆Siku ya Saba ni chanjo ya kwanza ya NEWCASTLE/ KIDERI-MDONDO
👉Muda huu wote watakua wanatumia chakula cha Starter/ Broiler starter.
WIKI LA PILI
👆Siku ya nane Hadi siku ya 12 Wapewe vitamins zipo Aina nyingi Sana Mfn :Aminototo, Farmvita, Dad OCTAVIT, Amylyte, Vitalyte n.k
👆Siku ya 13 wapewe maji matupu ( japo hata ukiwawekea vitamins si mbaya).
👆Siku ya 14 wapewe chanjo ya Pili ya Infections Bursal Disease / Gumboro
👉 Muda huu wote wapewe chakula cha Starter/ Broiler Starter.
WIKI LA TATU
👉Hapa tuna wagawa kuku kutokana na Aina
👆 KUKU WA NYAMA/BROILERS
👉Siku ya 14 au15 Hadi ya 22 wapewe Grower Pellets ( Kwa uzoefu wangu).
👆Hapa hawa kuku wanaweza kupewa Broiler Booster Mfn : Utravin broiler booster.
👆Siku ya 21 kuku Broiler wapewe chanjo moja wapo Kati ya Gumboro au KIDERI ( Hii inategemea MAZOEA ya namna ya kuchanja kuku kutokana na mkoa ulipo).
👉 KWA KUKU WANAOANDALIWAKUTAGA ( CHOTARA, LAYERS , KUKU WA KIENYEJI).
👆Wapewe chakula cha Starter Mashi inaenda mpaka wiki ya 7 au wiki ya 8 (inategemea maelezo ya chakula unachotumia na kampuni uliyo nunua chakula).
👉Siku ya 21 kuku hawa watapewa Chanjo ya pili ya Newcastle/KIDERI/MDONDO
👆Siku ya 28 kuku wanao andaliwa kutaga wapewe chanjo ya pili ya Gumboro
👆Siku ya 30-35 ni chanjo ya Ndui (Japo maeneo mengine Ndui hutokea mapema wiki ya 3).
👉Kila baada ya miezi mitatu kukuwako wapewe chanjo ya KIDERI/ Newcastle
KUMBUKA
👉 Minyoo ni hatari Sana Kwa maendeleo ya kuku....unapaswa kuwapa dawa za minyoo mapema Kwa mara ya kwanza wakifika miezi miwili , 👉Kisha utakua unarudia kila baada ya miezi mitatu USIPUUZE
👆Kwa chakula wape grower mash wiki ya nane au 9 mpaka wiki ya 18-19 ( Pale utakapo okota yai bandani).
NB : Kuku hawa wapewe vitamins mara Kwa mara ..sio lazima kuwapa kilasiku kupunguza Gharama
👆Kuku wako wakifikisha asilimia 3-5 za utagaji wape Layers mash moja Kwa moja Hadi pale utakapo amua kuja kuwauza
Ikumbukwe kuku hawa wanapaswa Kula Kwa kipimo maalumu kutokana na Umri
👆 MAZOEA YANAONESHA WATU KUFUGA KWA KUWEKA RATIBA YA DAWA KAMA CHAKULA
👉 Hii sisawa Kitaalamu , kuku wapewe dawa pindi wanapoumwa...Uzoefu wangu haunioneshi ulazima WA kukuza kuku Kwa Dawa.
Asante na karibu sana


5 Comments
Ahsante kwa elimu nzuri
ReplyDeleteAsante itumie
ReplyDeleteShukrani Kahise
ReplyDeleteKaribu naomba ufollow blog yangu
Delete👍👍👍👍👍👍 big up
ReplyDelete