*TUKUMBUSHANE KIDOGO*





 *Imeandaliwa* na 

Greyson Kahise

Mtaalamu wa kuku

0769799728

 *0715894582* 


Kama ilivo Kwa viumbe wengine, Chakula Bora, Afya njema, Utimamu wa Mwili ni njia Pekee, ya kuboresha au KUONGEZA uzalishaji Kwa MIFUGO hiyo,


 *Mfn* : Wakati Ng'ombe au Mbuzi anakamuliwa , huwa tunaweka chakula ale ili awe Sawa na *kutusaidia kutoa maziwa,  kama hutampa chakula muda huo atapunguza kiasi cha maziwa siku husika*


👏Hii haina utofauti Kwa mfugo *KUKU*, kuku ni kiumbe *Ndege* nae anahitaji matunzo Yale Yale Kwa KUTEGEMEA miongozo yake ili HATIMAE , AMA auzwe ndani ya Muda Kwa nyama, au *ATAGE* mapema mayai mengi na yenye size *yakueleweka*


👆🏿Moja ya malalamiko ambayo nimekua nikipokea mara Kwa mara kutoka Kwa wafugaji ni *Kuku kuvimba macho na kujaa kama tongotongo ndani au kutoa machozi*


👆🏿Ila ukiuliza Sana wafugaji Ratiba zao za kuwapa kuku vitamins zinatia *mashaka*, Mfn Mfugaji atawapa kuku wake vitamins hasa *wiki tatu* za Mwanzo na kuacha Hadi inapotokea *tatizo ndo anakuja kuanza kuwapa* tena , hii inakua si Sawa na unakua umechelewa sana.


🐓Nishauri Tu kwamba , vitamins Kwa kuku NI muhimu Sana, binafsi *KAHISE* Kwa uzoefu wangu nashauri kuku wapewe vitamins *Mfululizo* Tu bila Kuchoka wakiwa kwenye Brooding ( *Mwezi mmoja wa Kwanza)* 


👆🏿Kisha baada ya huo umri wa Mwezi mmoja , wa Mwanzo unaweza jiwekea utaratibu wa Kuwapa kuku Vitamin kila baada ya siku 10 *unawapa vitamins Mfululizo Kwa siku 5* Hii itakusaidia Sana kupunguza changamoto za magonjwa ya nayosababishwa na upungufu WA vitamins Mfano *AVITAMINOSIS*, au Encephalomalacia ( *Crazy chicks, kuku kuzungusha shingo kna kwamba ana mdondo* ).


Tukifanya hivo itatusaidia Sana kupunguza vifo vinavyo epukika.


 *NB*

👆🏿 :Usafi wa Banda muhimu Sana

👆🏿Usafi wa vyombo vya maji na chakula muhimu Sana

👆🏿Kuzingatia Ratiba za chanjo, dawa za minyoo na muda wa kulisha kuku muhimu Sana.

👆🏿Kulisha kuku kiwango sahihi na masaa ya Mwanga muhimu Sana.

👆🏿Kutunza kumbukumbu Muhimu Sana

👆🏿Kutumia wataalamu kwenye mradi endelevu wa kuku Muhimu Sana

👆🏿 *KULA NA KUENJOY MAISHA KWA BIDHAA ZA KUKU NDIO FAHARI YETU*


 *FANYA KAZI KWA BIDII ILA USISAHAU KULA NA KUISHI VIZURI*


Nitafute Kwa huduma zifuatazo

👆🏿USIMAMIZI WA MRADI WA KUKU

👆🏿 VIFARANGA

👆🏿USHAURI KUHUSU KUKU

👆🏿VITABU BORA VYA UFUGAJI WAKUKU

👆🏿FORMULA ZA CHAKULA CHA KUKU


 *KARIBUNI SANA I LOVE CHICKENS*